Monday 30 April 2012

MAPINDUZI YALIFANYIKA MWAKA 2007 WALIPOTUA DEAD PREZ SWAHILI-LAND


Mwaka 2007 ulikuwa ni mwaka wa faraja kwa wanaswahili hip hop nchini ,ni kipindi walipotua hip hop icons toka marekani DEAD PREZ pengine wengi wenu hili kundi ni geni maskioni mwenu lakini kwa wanahip hop wa miaka 90’ wanalitambua vizuri sana..DEAD PREZ walitua nchini kwa udhamini wa BIRITSH COUNCIL, hapo tunaweza sema ndio mapinduzi ya kwanza na yakweli kutoka kwa wasanii  nchini Tanzania, mapinduzi hayo yalifanywa na waasisi kutoka kundi bora la Swahili hiphop nchini TANZANIA ,KWANZA UNIT ndio…hakuna pingamizi juu ya hilo…likiongozwa na kiongozi wao Rhym-son au Chief Rhymson au Zavala pamoja na mwenzake Kibacha au K-Singo au KBC , Dead Prez waliongozwa na M-1 na Umi. dhumuni la ujio huo ulikuwa ni kuwapa  tumaini na kuhamasisha utamaduni na mwendo mzima wa hip hop nchini (Swahili hip hop) na tunajifunza nini ukilinganisha na mwenendo wa kwao marekani.. kilichogundulika ni kwamba swahili-land tunarasilimali za kutosha katika Nyanja nzima ya Swahili hip hop.


M-1 na Umi wanaounda kundi la DEAD PREZ kutoka marekani wakilianzisha na mapinduzi ndipo yalipoanza.
 
kuhusu kujifunza nilipata mahojiano na mkongwe wa swahili hip hop Imam Abbas hiki ndicho alichojibu” uumh…kwanza nimefurahi sana kuja kwa icons hawa ila pia napenda kuwakumbusha wapenzi wa swahili hip hop waelewe hili jambo tayari tunaandika historia ,kwamba wasanii wenyewe wameamua kuwaleta wanamapinduzi wenzao ni kama miujiza bigup to kwanza..ha ha ha kweli wao ni wa kwanza saluti, pili kushusu kujifunza na ujio wao kwanza wanajikubali kwamba wao ni wenzetu..na usaidizi unakuja wa kiitifaki zaidi ilikuboresha nguzo za hip hop kama mavunjo (breakdance),sanaa za kutumia mikono (grafitti)na zingine na pia kuwashawishi wadhamini watambue na waelewe hip hop ni tamaduni kama zingine kwa hilo nawapongeza Dead Prez .tatu waliokuja nayo sio mengi na sio mageni sababu sisi tulianza sikiliza hip hop tangu mwaka 1989 hivyo basi kikubwa sisi tunachokata ni connection tu za kupata record contract za kueleweka na kupata utambuzi kwenye asasi za kiserikali na zisizo-za-kiserikali ilikusonga mbele kama alivyo sema M-1, sababu tofauti yetu na wao ni lugha sisi kughani  Kiswahili na kiingereza wao kiingereza tu..,lakini tumejifunza sababu mtu hawezi toka mbali halaf usijifunze kitu itakuwa uongo….BIG UP DEAD PREZ…!!!”  


M-1 namiondoko ya kujigamba BRITISH COUNCIL.

Umi akishangaa watu walivyojitokeza  BRITISH COUNCIL.

Umi akibadilishana mawazo na mkali wa ragga nchini Zanzi-B.
Mkongwe KBC akiwa na Chidi Benz ,Kurasa ,Fid-Q na Lindu anachukua vipande vya luninga.

MAVUNJO pia yalikuwapo USIPIME.......

mdogo wake marehem D-Rob JLT pia akichukua vyake huku KURASA akinyoosha kidole kwa nyuma.

M-1 na shabiki wake.

YEEES..! Hiyo kali..... Umi akiwa na Joh Makini na Chidi Benz.

Na Kauli Mbiu ilikuwa "TUPO-PAMOJA" ndio bwana amani tu.

Usini sahau mi ndio AVERI...bwana(t-shirt nyeusi).
heavy weight M.C Prof.Jizzy na mshabiki wake.

KBC akilianzisha kulia kabisa Imam Abbas Fid-Q na Kurasa.

Tafakuri Mgavi Dosi Dr.Eibbas ,Adili na Kalapina wote ndani ya nyumba.

Lets Keep It Swahili Kati Kulia Zavala na Evans Bukuku.

Man-suli Akiwakilisha.

Randy'D'Dawn na mshabiki wake pia alionyesha luuuv...

Jamani na mie nimo...ha ha ha Mchomvu baby.....

SAIGON kalinye.. kalinye... kalinye oi oi oi oi....!!!!....oi oi mchomvu akisikilizia.

Dada yetu Enika hakuwa nyuma pia ndni ya nyumba.

We Mejah..!! umemaliza kazi manake bila ya wewe hapo mambo yote yameharibika..cheka kidogo ha ha ha ha pamoko sana.

Event Meneja wa Swahili hip hop family club LOCAL kati akijiachia na Prof.Jay na K-wa-Mapacha.

Ulidhani Rock City itakosa wewe....!! ,umejidanganya RADO Hapa.........!!!

Monday 23 April 2012

ENZI ZILEEEEE..........


MITAA YA KATI (Bila Sanaa Ningekuwa Mkabaji MitaaYa Kati)-Imam Abbas ft Juma Nature

 SAUTI YA KITAMBO KUTOKA MTAA
Hivyo ndivyo mashairi ya msanii mkongwe wa swahili Hip Hop, Imam Abbas yanavyoanza kwenye nyimbo yake ya ‘Bila Sanaa’ mwaka 1999. Nadhani lile swali la nini nafasi ya swahili Hip Hop katika jamii yetu litaanza kupata maana kupitia nyimbo hii. Pamoja na bado wapo wajinga wachache katika vyombo vya habari, wanaoita  swahili Hip Hop, muziki wa kufokafoka, bila kujua hii ni aina ya fasihi simulizi. Taswira ya fasihi katika nyimbo hii ni ya kipekee, ambayo inaibua maswali muhimu na kuonesha mustakabali wa vijana wa leo.

‘Bila sanaa’ inakupa mtazamo wa vijana walio wengi katika Tanzania ya leo, kwani maisha yao ni kama kuwa na “panga shingoni”. Panga hilo, laweza kuwa la kibaka akimwibia raia, au panga hilo laweza kuwa mafisadi wanaodhoofisha maendeleo; hivyo rushwa zao na ubinafsi wao ukizidi kuacha taifa lenye vijana wengi matatani.
Ugumu wa maisha, hasa kwa vijana unatokana na sababu mbalimbali. Wale walio bahatika, wakasoma na wenye vipaji, wanahemea kupitia elimu yao au sanaa yao, kama hii ya Hip Hop. Lakini wengi wa vijana wapo kwenye fungu la wanaoishi kwenye mazingira magumu na hatari. Hao sasa, ndio wale ambao kila siku wanatamani wangebaki “utotoni”, kwani “Bongo motoni;” kwani wakiwa wezi kweli watachomwa moto.
Lakini kwanini tuishi kama tupo motoni? Mtu unabaki ukijiuliza, hivi ukimya wetu vijana ndio unatufanya tuonekane mafala, au tumekubali yaishe kuwa sisi ni watu dhaifu. Labda moja kati ya sababu kubwa zinazotufanya tusiamke, ni hofu kuwa, kelele zetu “zitapotea kama moshi wa udi,” bila kusikiwa na hata kuleta mabadiliko yo yote.
Vijana waliosoma ni wachache, ajira zenyewe ni chache, na kwa wale ambao “maisha piga mashuti,” wanajikuta wanashindana na Wachina kwenye umachinga. Msanii II Proud enzi hizo aliuliza “ni wapi tunakwenda, tu.. tunakwenda” kipindi hicho ambapo tabia ya kuzamia meli kwa vijana ndiyo ilikuwa imeshamiri. Leo hii uzamiaji meli sio ishu tena, kwani tumekubali kubaki nyumbani na kuwa watumwa.
Sasa je, utumwa huu utakuja kufika kikomo? Hawa viongozi je, viongozi wanaodharau vijana, wanaodharau mchango wa swahili Hip Hop kwa vijana na jamii kwa ujumla, hivi hawajui hatari ya dharau zao? Leo hii, tunaweza kuulizana maswali tu, ya “tafakari je, ningevunja mlango wako, juu yake kibano, kisha vitu msanyo,” kupitia nyimbo hii. Lakini, kesho ufisadi ukazidi, maisha ya vijana yakazidi kuwa matatani, unadhani vijana tutabaki tu kuwa kwenye “kona ya mtaa,” huku moshi wa msuba unapaa, umeishia ukizubaa,” au hata wao mafisadi watajikuta wakiwa wamewekewa mapanga shingoni. Labda hilo ndilo tunalohitaji lifanyike, badala ya kugeuziana visu sisi wenyewe kwa wenyewe.

Bila ubishi, sisi vijana na hao mafisadi tuishukuru sanaa, kwani ‘Bila Sanaa’, Imam Abbas anajadili maisha yangekuwa vipi; labda angekuwa mkabaji, mteja, mwizi, muuaji, lakini pia Lupe Fiasco msanii wa Marekani ameweza kuandika baada ya miaka kumi, Hip Hop Saved His Life.basi upeo wa imam  utukuzwe.
Mwisho, Imam Abbas anaonya kuwa, “taifa la leo, majambazi wa kesho,” kama viongozi hawatachukulia kilio cha vijana kwa umakini. Kwani siku moja itatutabidi tujenge ukuta, wakati nyimbo kama ‘Bila Sanaa’, zinatuwekea wazi nyufa ambazo zinatakiwa kuzibwa. Mwisho wa siku, ukweli ni huu, matatizo ya vijana hayatatuliwa yote leo, kwani hata Roma haikujengwa kwa siku moja. Lakini sasa, juhudi lazima zianze leo, kwani kama nchi hii itateketea, basi sote tutateketea nayo, na tusisahau wala kudharau uwezekano huo.
Sikiliza nyimbo nyingine za Imam Abbas Horses na Sunshine. Pia unaweza kusikiliza wimbo wa Lupe Fiasco ‘Hip Hop Saved My Life…’

Friday 20 April 2012

wito kwa wote...sisi tunajali wewe je?

memba wa swahili hip hop family club Imam Abbas na Tuja wakibadlishana mawazo kwenye kituo cha mahabusu ya watoto upanga.
memba wa swahili hip hop family club faith,Tuja, Fanueli, Mwinyi, Natalia mlula na Alex Bwire  ambaye ni mlezi wa kituo cha mahabusu ya watoto upanga.


Mahabusu ya Watoto Upanga Tour

Shukurani za dhati kwa mtaarishaji wa muziki Lamar kutoka FishCrab Records,Emmanueli Okwi kutoka Simba Sports Club,Amir Maftah kutoka Simba Sports Club na Mejah Mbuya Wachata Crew kuungana nasi katika safari hii, bila kumsahau mkuu wa kituo Mzee.Alex Bwire

Amir maftah full-back wa simba akiwa kwenye mahabusu ya watoto upanga akitabasamu alipoingia watoto walipomshangilia.
membas wa swahili hiphop family club toka kushoto ni Tuja,Faith,Natalia ,Fanueli,Oscar,Randy'D'Dawn wakiwa kwenye mahabusu ya watoto upanga.
.

Wednesday 18 April 2012

Kutana na Randy 'D'Dawn na Album inkuja inaitwa"WELCOME'

Randall Seffu a.k.a Randy'D'Dawn ni msanii wa swahilihip hop yupo chini ya lebo ASAR ENTTERTAINMENT. yenye maskani yake mwenge ,kijana huyo anarekodi albmu chini ya studio za ZAKEY RECORDS na mtaarishaji Abdul Zakey zilizopo tabata/ilala, huyu kijana anasoma Kampala University  kilichopo ukonga Dar es salaam, hiyo albmu inajumuisha nyimbo 12 ambayo inaitwa "WELCOME/KARIBU " kaa chojo.....upishi umekamilika karibu albamu inaingia mtaani.

Monday 16 April 2012

swahili hip hop family club - kutembelea mahabusu ya watoto upanga

tunapenda kuwakaribisha members wetu wote kujumuika nasisi kutembelea gereza la watoto wadogo upanga siku ya alkhamis ya tarehe 19 mwezi huu saa 8
;00 mchana, tukiwa pale tutaweza kufurahi nao katika mambo mbali mbali, kufika kwako ndiyo furaha yao, karibuni sana.

Safari Moja, Sauti Moja........Umoja ni Nguvu.